Pages

MY NEW FILM TRAILER INAITWA ''DR MAX''

Thursday, November 21, 2013

EXCLUSIVE KUHUSU MINI ZIFF 2013 NA FILAMU ZA BONGO:

MINI ZIFF 2013 inafanyika sambamba na Sherehe za miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar. Tamasha hili dogo litafanyika tarehe 10 -12 Jan, 2014 na kama kawaida ZIFF itatoa tuzo 10 za Filamu kwa waliofanya vizuri kwa mwaka 2013 katika filamu za Kiswahili (Bongo Movie). Tuzo zitakazotolewa ni Muigizaji Bora wa Kiume na Kike, Muongozaji Bora, Filamu Bora ya Mwaka, Muigizaji anayechipukia, Filamu bora katika Sauti, Filamu bora katika Hadithi, Balozi bora wa Filamu za kitanzania, Kampuni au mtu aliyetoa mchango mkubwa katika Tasnia hii kwa mwaka huu na Tuzo ya Heshima. Tamasha hili dogo litajumuisha filamu za kitanzania peke yake (Bongo movies) ilikuendelea kutoa mwamko kwa watengenezaji filamu wa Tanzania kufanya vyema katika tasnia hii, Tamasha hili ni utangulizi wa tamasha kubwa la ZIFF litakalofanyika 14 – 22 Juni, 2014.

Tuzo zitatolewa baada ya jopo la majaji kupitia kazi zilizoletwa kwaajili ya Mini ZIFF na pia Tuzo ya Muigizaji Bora wa Kiume na Kike zitapata kupigiwa kura na wananchi kupitia namba maalum itakayotolewa hapo baadae kupitia Puch Mobile na hivyo kufanya watu wote Tanzania nzima kupiga kura.
Mini ZIFF itaonesha filamu kwa siku mbili na siku ya mwisho Tuzo zitatolewa kwa walioshinda, pia tunategemea kuwaalika wasanii mbalimbali maarufu kutoka hapa Tanzania kama JB, Cloud, Steve Nyerere, Ray, Makombora, Simon Mwakifamba, Monalisa, Wema Sepetu, Irene Uwoya, Lulu na wengine wengi.
Pia tunategemea kufanya show kabambe ya muziki baada ya kutolewa kwa tuzo, wasanii watakaopanda jukwaani watatangazwa hapo baadae. Kwa wale wote wanaotaka kuleta kazi zao basi walete sasa ila ziwe ambazo zimetoka mwaka 2013 tu. Wasiliana na Ibra 0713300997(DAR) au Mohd 0778685676 (ZNZ).
MINI ZIFF 2013 inaletwa kwa udhamini mkubwa wa ZUKU, Push Mobile, Azam Marine, Filamu Central Clouds TV kupitia kipindi cha Take One na Clouds FM kupitia kipindi cha Leo Tena.



TOA MAONI YAKO HAPA:

MWANA MUSIKI LINEX KUONEKANA KWENYE FILAMU HII:

Msanii Linex Sunday Mjeda aka The V.O.A ameamua kufungua ukurasa wa pili wa kipaji ambacho hajawahi kukionesha cha uigizaji, hivi karibuni ataonekana katika filamu mpya ya muigizaji wa bongo movie Aunty Ezekiel inayoitwa ‘MWAJUMA’.
Kwa mujibu wa tovuti ya bongo5, linex ameeleza kuwa  filamu ya Mwajuma inahusu mwanadada aliyekuwa na maisha ya chini akiwa mama ntilie na baadae kuja kufanikiwa na kuanza maisha ya kihuni hususani kubadilisha wanaume kama nguo
Filamu hii inatarajiwa kutoma mwishoni mwa mwezi ujao


TOA MAONI YAKO HAPA:

Thursday, November 14, 2013

WEMA AWAPONDA WALIO KACHA MSIBA WA BABA AKE, ASEMA SIO WOTE NI:

Kupitia kipindi chake cha ‘In My Shoes’ cha jana, Wema Sepetu alieleza jinsi alivyojisikia baada ya baadhi ya waigizaji wenzie wa Bongo Movie kugoma kuhudhuria msiba wa baba yake, Balozi Isaac Abraham Sepetu, mwishoni mwa mwezi uliopita kwa madai kuwa yeye hakuwa akifanya hivyo kwenye misiba mingine.
“Imeshatokea, wameacha kuja kwenye msiba, ni wao,” alisema Wema. Sio Bongo movie nzima, ni baadhi tu ya watu ambao wanauelewa na upeo mdogo ambao waliamua kutokuja. Lakini niliona Bongo movie wengi, walikuwepo marafiki zangu wengi, akina Batulli, akina Esha, Wolper alikuja, Lulu, JB alikuja, Jokate alikuja, Adam Kuambiana alikuja. Ambaye napenda nimpe my special thanks and appreciation, ambaye alijitolea from the beginning wa msiba mpaka to the end ni Dokta Cheni kwakweli. Dr Cheni, I thank na ntazidi kumshukuru,” alisema.
“Marafiki zangu kama akina Kajala, akina Zamaradi, wale sio marafiki, wale tayari ni ndugu, kwahiyo siwezi kuwaweka kwenye appreciation wala kwenye thanks.”
Katika kipindi hicho pia, Wema alisema yeye na ndugu zake walijua kuwa baba yako ni muumini wa dhehebu la Roman Catholic siku chache kabla ya kufariki dunia.
Balozi Issac Abraham Sepetu (71), alizikwa kikristo katika kijiji cha Mbuzini,mkoa wa Kusini Unguja October 30 ambapo mazishi yake yalihudhuriwa pia na Rais wa Zanzibar,Dk Ali Mohammed Shein pamoja na viongozi wengine. br />


TOA MAONI YAKO HAPA:

Tuesday, November 12, 2013

SABABU ZA IRENE UWOYA KUJIFUA MAZOEZI KWA MATUMLA.

MSANII wa filamu wa kike Bongo Irene Uwoya yupo katika maandalizi ya kuanza mazoezi ya ngumi baada ya kumpata mwalimu ambaye ni Bondia maarufu Rashid Matumla ‘Snake Boy’ akiongea na FC Irene kasema kuwa ameamua kufanya mazoezi kwa ajili ya kujiweka vema na kulinda nafasi yake ya uigizaji kwani amegundua wasanii wengi wanapoteza mvuto kwa kujiachia kwa unene.

“Nimejipanga kwa kufanya mazoezi ya nguvu chini ya mwalimu wangu Rashid Matumla na nipo fiti kwa ajili ya kujifua najua kuigiza ndio ajira yangu lakini nikijiachia na kunenepa bila mpango nitaanza kucheza nafasi za akina bibi muda si mrefu na najiona mwili
unavyoninyemelea sitaki manyama uzembe,”anasema Irene Uwoya.
Irene ni moja kati ya wasanii wakali wanaofanya vizuri katika tasnia ya filamau Bongo huku pia akiwa ni moja kati ya watayarishaji wa filamu wanadada akiwa ameandaa filamu la Apple filamu iliyotengenezwa kwa gharama kubwa na kuwashirikisha wasanii kama Patcho Mwamba, Baba Haji na wasanii wengine wanaofanya vizuri katika tasnia ya filamu Bongo.


TOA MAONI YAKO HAPA:

Monday, November 11, 2013

JACQUELINE WOLPER AFUNGUKA BAADA YA KUBADILI DINI KWA MARA YA PILI;

Hatimaye mwanadada Jacqueline Wolper ameamua kuweka wazi kilichotokea mpaka kuamua kubadili Dini yake ya Uislamu na kurudi kwenye ukristo tena. Kupitia ukurasa wake wa mtandao mmoja wa kijamii mwanadada huyu wa bongo movies ametoa ujumbe ufuatao kwa mashabiki wake.
“…mambo mashabiki zangu.sikua na njia nyingne yakulikwepa hili nanaamini kua kwa wale mashabk zangu waislam amtomaind maana akuna mtu wakumsikiliza chin ya hanga zaidi yawazazi so imenipasa kurudi kanisani kwakauli yawazazi wangu.naamin kama aujaolewa ata uwe na miaka mingap bado unatakiwa kua chin ya imaya ya wazazi ata ukifa ujue unazikwaje na mimi ni binadam sijui saa wala dakika.muhm nikuwajuza nakuwaelewesha mashabk zangu stak maswal nawapenda wote…”
Hapo awali iliripotiwa kuwa mwanadada huyu ameamua kuwa mkristo tena baada ya penzi lake lililosababisha abadili dini na kuwa muislamu na jamaa aitwaye 'Dallas' kuvunjika hivi karibuni.
Swali ni je, atabadili dini tena akitokea mwingine wa dini aliyo tofauti na sasa? br /> (imetoka Bongomovies)
TOA MAONI YAKO HAPA:

Saturday, November 9, 2013

TUSIMLAUMU RAY,WEMA ALIKUA HAJITOI KWENYE MISIBA YA WENZAKE;''STEVE NYERERE''

Tusimlaumu Ray; Wema alikuwa hajitoi kwenye misiba ya wenzake- Steven Nyerere
Msanii wa filamu, Steve Nyerere amesema Wema Sepetu alikuwa hajitoi kwenye matatazo ya wasanii wenzake wa filamu na ndio maana wasanii wengi wa filamu wakashindwa kuhudhuria katika mazishi ya baba yake, Balozi Isaac Abraham Sepetu mwishoni mwa mwezi uliopita.

Akizungumza  leo Steve,amesema anawataka watu waache kumtupia lawama Vicent Kigosi aka ‘Ray’ wakati mwanadada huyo alikuwa hahudhurii katika matatizo ya wenzake.

“Mnamlaumu bure Ray jambo ambalo hajafanya kwakuwa Ray ni jalala basi kila kitu mnamtupia,jamani mwacheni apumzike,” amesema Steve.

“Sisi katika Bongo Movie Unity tuna uongozi, tuna mwenyekiti,tuna mwenyekiti wa mipango ambaye ndio mimi, na tuna makamu wa mwenyekiti ambaye ndio mimi na tuna makamu mwenyekiti ambaye ni Irene Uwoya. Lakini sisi taratibu zetu kwenye misiba kama unaona kwenye misiba yetu tunajitoa,lakini linavyotufika tunaangalia ni mwanachama gani naye anakua anajitoa katika misiba ya wenzake

TAMASHA KUBWA LA EUROPEAN FILM FESTIVAL KUANZA 22.NOVEMBER 2013.

EFF 2013
Tamasha kubwa la Filamu( European Film Festival)
TAMASHA kubwa la filamu ambalo ufanyika kila mwaka la European Film Festival (EFF2013) lipo tayari kwa mwaka huu na litaanza rasmi tarehe 22 November 2013 kwa kuonyeshwa filamu mbalimbali katika vituo vilivyopangwa ambazo ni Alliance Francaise, Mlimani City Century Cinemax, Goethe-Institut na Nafasi ArtSpace filamu zitaonyeshwa kwa siku tatu tarehe 22, 23 na 24 November 2013.
Tamasha la European film Festival 2013
 Eff 2013
Tamasha la hili limekusudia kuinua tasnia ya filamu ya Tanzania katika kujifunza utamaduni kutoka Ulaya katika njia ya filamu katika kuimalisha na kukuza utamaduni wan chi husika hivyo ni njia nzuri kwa watengeneza filamu wa Swahiliwood kushiriki katika kujifunza zaidi utengenezaji bora wa filamu.
Filamu nzuri na za kusismua kama vile Limbo, Kings, Tea or Electricity, The Great bear na nyinginezo zitaonyeshwa katika kujenga na kutoa nguvu sambamba na elimu burudani kutoka katika filamu husika, ni tamasha muhimu sana kushiriki kujionea tasnia kutoka Ulaya ilivyopiga hatua, KINGILIO NI BURE unaweza kutembelea

Tuesday, November 5, 2013

LOWASSA ANGURUMA BUNGENI:


Edward Lowassa.
Katika hali isiyo ya kawaida, Waziri Mkuu aliyejiuzulu, ambaye huongea kwa nadra bungeni, Edward Lowassa leo amenguruma na kutaka taifa kuacha kuweka vipaumbele vingi visivyotekelezeka kwa wakati.
Alitaka serikali kuweka nguvu katika vipengele vichache vya msingi kama ajira, afya, elimu na miundombinu.
Aliwapongeza mawaziri John Magufuli kwa kuimarisha barabara na Dk. Harrison Mwakyembe kwa kubuni mbinu za kupunguza foleni jijini Dar es Salaam, alizosema zinachangia kuharibu uchumi kwani watu wengi wanakaa barabarani badala ya kufanya kazi.

Monday, November 4, 2013

SHAROBARO ALA KICHAPO KISA MKE WA MTU


 Kwa vile mke wa mtu sumu nimeona ni bora ni share na nyinyi watu wangu hii habri isome kwa kituo
 Issa Mnally Na Richard Bukos(gpl)
KIJANA mmoja mtanashati ‘Sharobaro’ ambaye jina lake halikuweza kupatikana mara moja juzikati alijikuta akichezea kichapo cha mbwa mwizi kisa kikidaiwa kuwa ni mke wa mtu.

Usione vyaelea: Sharobaro (katikati) akilia baada ya kuchezea kichapo kwa kukutwa na mke wa mtu.
Tukio hilo lilijiri saa saba usiku mwishoni mwa wiki iliyopita, Chalinze mkoani Pwani ambapo mapaparazi wetu walikwenda kwa ajili ya uzinduzi wa kundi jipya la sanaa liitwalo 3 Ways.
Wakati shamrashamra zikiendelea, ghafla liliibuka timbwili na katika kufuatilia ilibainika sharobaro anayeishi eneo hilo alikuwa

Sunday, November 3, 2013

MKE WA WILLIAM AJIFUNGUA MTOTO WA KIKE: soma zaidi hapa;

Mke wa William Mtitu ajifungua mtoto kike. Soma zaidi hapa
Mwigizaji, muongozaji wa filamu na mmiliki wa kampuni wa filamu ya 5effects William Mtitu amepata bahati ya kuongeza idadi ya wanafamilia wake baada ya mke wake Jovitha Mtitu kujifungua salama mtoto wao wa kwanza kwenye hospitali ya Regency jijini Dar es salaam hivi majuzi.
Kupitia ukurasa wa mtandao mmoja wa kijamii Mtitu aliandika…
“Nawashukuru madaktari wa hospital ya regency na kwa Dr mvungi wakiongozwa na Dr getu kwa kusaidia mpaka mke wangu kujifungua salama na sasa naitwa baba na mke wangu mama ,kwa kweli mungu awabaliki sana…”
Hali ya Mama na mtoto ni njema na  wanaendelea vizuri. Hongera sana Mtitu na familia yako.
(imetoka Bongomovies)
TOA MAONI YAKO HAPA:

''NAPUMZIKA KUIGIZA FILAMU ZA BONGO ZINAFANANA''- ROSE NDAUKA

Filamu za bongo zinafanana sana. Napumzika kuigiza - Rose Ndauka
 (imetoka BongoMovie)
Mwigizaji Rose Ndauka amesema kuwa anapumzika kwenye tasnia ya filamu kwa mwaka mmoja kwakuwa filamu za Tanzania zinafanana sana na anataka aje na kitu kipya na tofauti.
Kwa mujibu wa gazeti la mwanaspoti Rose Ndauka amesema wazo hilo limetokana na tatizo la kufanya kazi zinazojirudia mara kwa mara, hali iliyomfanya aamue kujipa likizo ya muda ili kujipanga.
Hata hivyo kauli hiyo inaweza kuwa na utata muigizaji huyo ni mjamzito kwa sasa na huenda hiyo ndio ikawa ni sababu kubwa ya yeye kusimama kwa muda.
TOA MAONI YAKO HAPA:

Friday, November 1, 2013

Baba Kanumba ampiga marufuku mama kanumba jina la Kanumba.




Katika hali ya kushangaza, baba wa aliyekuwa msanii maarufu wa filamu Bongo, marehemu Steven Kanumba, Charles Kanumba amempiga marufuku mama mzazi wa msanii huyo, Flora Mtegoa kutumia jina la Kanumba kwa namna yoyote.
Akizungumza na Ijumaa hivi karibuni baba Kanumba alisema mama Kanumba hana mamlaka ya kulitumia jina la Kanumba kwani hana uhusiano nalo.
“Mimi ndiye mwenye mamlaka na jina la Kanumba kwa sababu ni la kwangu lakini namshangaa mama Kanumba kuendelea kulitumia jina hilo hata kwa watoto wasionihusu kama mtoto wa mwanaye aliyezaliwa hivi karibuni na kuitwa Kanumba Junior
“Anahusiana nini na hilo jina wakati huyo siyo damu yangu, yeye ana baba yake kwa nini asitumie jina lake, sitaki kabisa atumie jina langu mwanangu ameshafariki na mimi ndiye mwenye mamlaka ya kutumia hilo jina,” alisema mzee huyo.
Akilizungumzia suala hiyo, mama Kanumba alisema: Sitaki kumsikia kabisa,kama vipi aende mahakamani.”
TOA MAONI YAKO HAPA:

Tuesday, October 29, 2013

RATIBA YA MAZISHI YA MAREHEMU MZEE SEPETU NILIYOIPATA:

RAY:
Habari zenu ndugu zangu, i hope mmeamka salaama salamin, kwa wale wagongwa allah atawaafu inshaallah:
Tangu juzi nimekua nikishare na nyinyi taarifa za Msiba wa Baba Mzazi wa Mwanafilamu mwenzangu WEMA SEPETU mzee ABRAHAM SEPETU:
Taarifa hizi nazipata kutoka kwa Ndugi wa Karibu wa Wema Sepetu ambae ni Binamu yake anaeitwa RAY ambaye ni Mkurugenzi wa Bendi ya Cococnut Zanzibar;
Ratiba YA Mazishi yatakavyo kua Kisiwan Zanzibar:
PICHA YA MAREHEMU ABRAHAM SEPETU ENZI ZA UHAI WAKE:
''Maiti itaondoka na Boti ya Kesho Asubuhi kuelekea Zanzibar na Kufikishwa Moja kwa moja kanisani kwa misa fupi kisha baraza la wawakilishi la Zamani, kwa waheshimiwa kutoa heshima zao za mwisho.Baada ya hapo msafara utaelekea nyumbani kwake Mbuzini kwa ajili ya Mazishi:''
kama kuna chcochote kitakacho badilika tutajulishana hapa hapa:
Ahsanteni Endelea kutembelea blog hii na Uwaambie wengine pia:
R.I.P Mzee Abraham Sepetu
TOA MAONI YAKO HAPA:

Sunday, October 27, 2013

TAARIFA JUU YA KIFO NA MAZIKO YA BABA WA WEMA SEPETU (MZEE ISSAC SEPETU)

Leo mapema tumepokea taarifa za kifo cha Baba mzazi wa Msanii nguli wa Filam nchini Tanzania Wema Sepetu Mzee Issac Sepetu (pichani), Ambae alikua anaumwa na amelazwa katika hospitali ya TMJ jiji Dar,Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Band Ya #COCONUT BAND ya Zanzibar Bwana RAY ambae ni  ndugu na wema sepetu ba mkubwa kwa ba mdogo, alisema mwili wa mzee sepetu kwa sasa umeshapelekwa katika Monchwari ya hospital Kuu ya Muhimbili:
Alipotakiwa kusema kuhusu wapi na nilini atazikwa mzee huyo: Bw; Ray alisema
Ray Mkurugenzi wa Coconut Band Zanzibar:
''kwa sasa tunawasubiri baadhi ya watoto wake waliyokuwepo marekani wafike, na wengine waliyokuwepo ujerumani na tunatarajia watafika kwenye jumanne, sasa wakifika tutazika kati ya juma nne au juma tano, na mzee tunatarajia atazikwa kwenye shamba yake Visiwani Zanzibar iliyoko shamba Mbuzini''
TOA MAONI YAKO HAPA:

Wednesday, October 23, 2013

(VIDEO) TRAILER FILAMU MPYA YA CLOUD 112 ''DR MAX''

Tumshkuru muumba kwa kutujaalia kumaliza salama kile ambacho mlitutuma kukifanya Timu nzima ya CY & CL COMPANY  Tmemalizaq kwa salama na Amani sasa imebakia zamu yenu tuu kukiangalia kile ambacho tulikua tunakifanaya, Filam Yetu ya DR MAX imemaliza Licha ya changamoto za hapa na pale, 
kua wa kwanza angalia hapa Trailer ya Filamu hii hapa pekee, then utatupa comment yako hapo chini:#
ASNTENI kwa Kuwa na sisi mpaka leo kwa support zenu: asanteni sana angalia hapa Trailer;
 
TOA MAONI YAKO HAPA:

ANGALIA HAPA SEHEMU YA KWANZA YA KIPINDI CHA WEMA SEPETU

Kile kipindi kilichokuwa kikisubiriwa kwa hamu na wapenzi wa filamu nchini , “Wema Sepetu Reality show” kwa mara ya kwanza kimeruka hewani kupitia kituo cha TV cha EATV  hapo jana.
Katika episode hii ya kwanza, Wema amejitambulisha nan  kuelezea historia yake kwa ufupi kukusu yeye.

TOA MAONI YAKO HAPA:

Monday, October 21, 2013

Tughe wataka Zitto achukuliwe hatua kwa kutaja mshahara wa rais

 (HABARILEO)
HATUA ya Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe kutaja hadharani mshahara wa Rais na Waziri Mkuu, imechukua sura mpya baada ya Chama cha Wafanyakazi wa Serikali Kuu na Afya (TUGHE) kulaani hatua hiyo na kuomba Spika Anne Makinda kuchukua hatua kwa vile ni ukiukaji wa sheria.
Chama hicho kimeeleza kusikitishwa na kitendo hicho kufanywa na Mbunge aliyehusika na upitishaji wa sheria hiyo huku wabunge wenyewe wakiwa wakali pale wananchi na wadau mbalimbali wanapohoji mapato yao.
Katibu Mkuu wa Tughe Taifa, Ally Kiwenge alisema Dar es Salaam jana kwamba pamoja na hatua hiyo kukiuka sheria ya kazi na uhusiano kazini inayosema mshahara ni siri ya mwajiri na mwajiriwa, pia kitendo hicho si ajenda ya wafanyakazi hivi sasa.
Alisema ajenda ya wafanyakazi kwa sasa ni kuona wabunge wanapigana kufa kupona katika kuhakikisha kuwa mshahara wa mfanyakazi unaongezeka kukidhi mahitaji ya mwezi mzima na kuwaondolea mzigo wa mikopo inayowaandama.
“Huu si wakati wa wafanyakazi kutaka kujua mishahara ya Rais au Waziri Mkuu, ajenda yetu kwa sasa ni kuona wabunge wanapigana ili kuboresha mishahara ya wafanyakazi ili ukidhi mahitaji muhimu tofauti na sasa,” alisema Kiwenge.
Alisema pamoja na hilo ni mkakati wa wafanyakazi sasa kuona wabunge wanatumia muda wao uliosalia kabla ya Bunge kuvunjwa kuhakikisha mambo makubwa mawili yanaingizwa katika Katiba mpya, moja ikiwa ni nafasi ya mfanyakazi kikatiba ikoje na pia kuona Katiba mpya inasema nini juu ya hatima ya maslahi ya wafanyakazi.

KIANGALIE KIKOSI CHA YANGA KITAKACHO IVAA SIMBA LEO:

Kama tujuavyo leo kuna mechi kali sana kati ya wapinzani wa jadi, SIMBA na YANGA, ahadi kede kede zimewekwa na wachezaji pamoja ana mashabiki wa timu hizo mbili, majigambo pia tumeyasikia kutoka kwa wachezaji pamoja ana mashabiki wa timu zote mbili, lakini tunavyoamini sisi ni kwamba mpira Dakika tisini,Kabla hujafika hebu chukua time kuangalia list ya YANGA, itakayoingia uwanjani pamoja na Reserve wake hapa:

Friday, October 18, 2013

WASTARA AUMIA MGUU TENA NAIROBI:

Na Gladness Mallya(gpl)
MWANADADA anayeendesha maisha yake kwa kuuza nyago kwenye filamu Bongo,  Wastara Juma ameumia mguu baada ya kuwekewa mwingine mpya wa bandia huko Nairobi nchini Kenya.

 Akizungumza na paparazi wetu siku chache baada ya kurudi Bongo, Wastara alisema aliumia wakati akifanya mazoezi ya mguu mpya aliowekewa ambapo kwa sasa anaendelea kuuguza jeraha hilo na amerudi mara moja kwa ajili ya Sikukuu ya Idd, ikimalizika atarejea tena nchini humo kwa ajili ya matibabu zaidi.
“Nimeshindwa kula sikukuu mbali na watoto wangu ndiyo maana nikaja mara moja japokuwa siko vizuri kwa sababu niliumia kwenye mazoezi ya kutumia mguu mpya huko Nairobi  na sasa nauguza kidonda lakini baada ya hapo nitarudi tena Nairobi kwa ajili ya matibabu,” alisema Wastara.
TOA MAONI YAKO HAPA:

WADAU WABARIKI NDOA YA WEMA SEPETU, DIAMOND:

Na Shakoor Jongo(GPL)
Wadau na mashabiki wa mastaa wawili nchini, Wema Sepetu wa Bongo Movie na Nasibu Abdul ‘Diamond’ wa muziki wa kizazi kipya, wamebariki ndoa ya wapenzi hao kwa kusema kuwa ni watu wanaoendana na kutegemeana kwa kiasi kikubwa.

Mwanzoni mwa wiki hii, Wema na Diamond walitupia katika kurasa zao za mitandao ya kijamii picha zao, ambazo zinaonekana zilipigwa eneo moja kwa simu moja na hivyo kuwapa wakati mzuri mashabiki wao ambao walionekana kupendezwa na uhusiano wao na kupendekeza waoane.
“Hii ndiyo couple bomba zaidi ya wasanii Bongo, kwa nini msioane? Mnapendeza sana jamani, ebu Diamond Platnumz achana na Penny bwana, huendani naye kwanza kuna mambo ya

Monday, October 14, 2013

JAY Z ALIVYOJICHANGANYA NA RAIA KWENYE TRENI:

 PICHA/Story TimesFm
Unaikumbuka ile surprise ya Mheshimiwa Mwakyembe kujichanganya kwenye treni ya abiria bila kutoa taarifa? Eeh..sasa Jay Z naye amefanya yake japo malengo yao yanatofautiana.
Rapper mwenye utajiri mkubwa na ulinzi wa kutosha amewasuprise fans wake wa London baada ya kujichanganya nao kwenye usafiri wa treni  wakati anaelekea kwenye tamasha lake katika eneo maarufu kwa burudani na sanaa ‘O2’ lililoko kusini mashariki mwa jiji hilo.
Ripoti toka katika nchi ya Malkia Elizabeth zinasema baba Blue Ivy ambae yuko jijini London ikiwa ni kati ya ratiba ya Magna Carta World tour, jumamosi jioni alipanda treni kama abiria wa kawaida akiwa ameongozana na

MAMA DIAMOND AINGILIA PENZI LA DIAMOND, WEMA


Stori: Mwandishi Wetu/Gpl
MAMA mzazi wa mkali wa ngoma ya Number One, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Sanura Kasim ‘Sandra’ ameingilia kati penzi lililofufuka upya kati ya mwanaye na staa wa filamu za Kibongo, Wema Sepetu.
Habari za chini ya kapeti zilitonya kuwa baada ya kuambiwa na kuoneshwa picha za Diamond akiwa kimahaba na Wema alikuja juu akidai kuwa hamtaki Wema kwa kuwa anamkubali zaidi Penniel Mungilwa ‘Penny’.
Akizungumza na Ijumaa Wikienda nyumbani kwake Sinza-Mori jijini Dar wikiendi iliyopita, bi’mkubwa huyo alisema kuwa kwa sasa hafahamu chochote kuhusu Diamond kurudiana na Wema zaidi ya kusikia kwa watu na kuona picha katika mitandao ya kijamii.
“Kuhusu Nasibu (Diamond) kurudiana na Wema, nasikia tu na kuoneshwa picha namsubiri Nasibu arudi kisha nikae naye ndipo nitatoa tamko,” alisema

Saturday, October 12, 2013

HAMMY B JAJI MPYA TUSKER PROJECT FAME TPF6:

 By EATV
Waandaaji wa shindano la kusaka vipaji vya kuimba lijulikanalo kama Tusker Project Fame hii leo limemtangaza jaji mpya wa mashindano hayo kutoka Tanzania.

Kwa mujibu wa Meneja wa Tusker Bi.  Bi Sialouise Shayo amesema kuwa jaji ambaye amechukua nafasi ya Mzee Zahir Zoro ni  Hermes J Bariki Hermy B.

Kwa upande wa mzee Zahir Zoro amesema kuwa amewapitisha vijana wanne ambao ana uhakika wataipeperusha vyema bendera ya Tanzania.


Naye Hermy B ameahidi kutekeleza majukumu yake ipasavyo kwani ana uzoefu na mashindano hayo kwa muda mrefu.
TOA MAONI YAKO HAPA:

RAMA DEE: NAFASI YA R&B NI KUBWA SANA TANZANIA:

 by TIMESFM
Inawezekana we pia ukawa mmoja kati ya watu wanaoamini kuwa nyimbo zenye temple zinazokimbia sana ndio zinazopendwa zaidi Tanzania, au kama we ni msanii unawaza kuhama R&B ufanye  ngoma inayokimbia kama ya…, lakini Mwimbaji wa R&B Rama Dee yeye anaamini R&B ina nafasi zaidi nchini Tanzania na kwa anashauri usipokee maoni ya marafiki zako tu, ila uangalie pia watu duniani wanasikikiliza nini .
Hit Maker wa ‘Kama Huwezi’amefunguka kupitia kipindi cha The Chat cha Timesfm kinachoendeshwa na Ezden The Rocker kila jumamosi saa nne kamili asubuhi hadi saa sita kamili mchana.
“Nafasi ya R&B ni kubwa zaidi Tanzania, usiangalie tu rafiki zako wanasikiliza nini angalia watu duniani wanasikiliza nini halafu utapata jibu zuri zaidi, kwa hiyo R&B ina nafasi nyingi hata kama haina nafasi labda Tanga, ama labda haina nafasi Bukoba lakini ina nafasi zaidi Dar es Salaam na mikoa mingine na labda nchi nyingine tofautitofauti, kwa hiyo opportunities zipo nyingi sana, na wasanii wapo wengi sana wanafanya vizuri na wanafanya na live band, kama akina Damian, The Voice pia wapo, kwa hiyo mi naamini baada ya labda mwaka mmoja kila kitu kitaanza kutoka na kuonekana .” Amesema Rama Dee.
Wimbo wa Rama Dee aliomshirikisha Lady Jay Dee ‘Kama Huwezi’ umeshika nafasi ya 8 kwenye The Chat Countdown yenye nyimbo 20.

TOA MAONI YAKO HAPA:

Thursday, October 10, 2013

PICHA ZILIZOVUJA ZA WEMA NA DIAMOND WAKIWA MJINI MALAYSIA:

Katika kile kinachoendelea mitandaoni, kuhusia na Stars wawili, waliyowahi kuwa wapenzi hapo awali, ni kwamba eti wamerudiana, japo kua Diamond alishatoa Tamko juzi kwamba hakuna mapenzi ya aina yoyote, yanayo muhisha yeye na mwnadada wema lakin, Ghafla Picha za wawili hao wakiwa Nchini MALAYSIA ambako Diamond alienda kufanya show Kipindi Flan hivi zikaanza kuvuja,
Hebu na wewe pata kuzishuhudia picha hizo ingawa Diamond amesema ni Filam Mpya ambayo amecheza yeye na wema, sasa wewe ndio utakua Jaji: mimi simo::

Wednesday, October 9, 2013

COVER YA FILAMU YANGU MPYA YA DR MAX ICHEKI HAPA:

MAELEZO:
''Filamu ya Dr Max, ni Filamu ya Kitanzania inayomzungumzia Dr Max ambae anaamua Kufuta Hatua Kadhaa alizopiga na Kusonga mbele, Lakini hakumbuki kuawa kusonga mbele bila ya Kufuta Dosari za nyuma ni sawa na kuanza tena Safari ya Kurudi nyuma:'
TOA MAONI YAKO HAPA:

Tuesday, October 8, 2013

HIZI TAARIFA ZA MZEE MAJUTO KUGOMBEA UBUNGE 2015;

 (habari/BongoMovies)
Habari tulizozipata zinasema kuwa gwiji la sanaa za vichekesho nchini, Amri Athumani 'King Majuto' ametangaza kugombea ubunge kwa 2015.
Muigizaji huyu mkongwe mzee Majuto ametangaza  kugombea ubunge jimbo la Tanga mjini.
Majuto  mwenye umri  zaidi ya miaka 60 ametangaza nia yake hiyo alipohojiwa na Clouds, na akadai atagombea kupitia CCM.
Bado tunamtafuta mzee majuto ili aweze kututhibitishia kama habari hizi ni kwa kweli au la na kama ni kweli ana mipango gani na jimbo hilo la Tanga mjini.
Je, kama ni kweli, unahisi ataweza ? Tupe maoni yako
TOA MAONI YAKO HAPA:

Monday, October 7, 2013

Washiriki wanne wanaoiwakilisha Tanzania kwenye Tusker Project Fame

Tusker project fame mashindano ambayo yamewahi kuwapa ustaa wasanii kama Hemed PHD wa Tanzania yamefikia hatua ya washiriki kukaa kwenye academy ambapo matumaini ya Watanzania kufanya vizuri kwenye mashindano haya yapo mikononi mwa watu wanne.
Watu wenyewe ni  Angel, 23 yrs, Hisia 21 yrs, Tanah 21 yrs na Dubson 25yrs, unaweza kufatilia show ili ujue jinsi ya kuwapa support Watanzania hawa mtu wa nguvu ambao wako kwenye list ya zaidi ya wasanii 15 kutoka nchi mbalimbali za Afrika Mashariki.


TOA MAONI YAKO HAPA:

BARAFU ATOA YA MOYONI KUHUSU VIPAJI VYA MTAANI:

BY  filamucentral
MWIGIZAJI na mtayarishaji wa filamu Swahiliwood Suleiman Barafu ametoa kali pale alipoongelea soko la filamu la Bongo kwa kuwalaumu baadhi ya wasanii ambao hajawataja majina kwa kusema kuwa wasanii hao wapo katika tasnia ya filamu kwa muda mrefu kiasi cha kuona fani hiyo ni mali yao na hakuna anayestahili kuingia au kuigiza.
“Katika soko la filamu kuna tabia ya kubaniana, wasanii wakongwe hawataki kizazi kipya, kila sehemu wanataka wao pamoja na kuwa hawawezi, unamkuta mtu akipewa nafasi ya kukuongelea kwa bosi anakuponda mwanzo mwisho, sasa na sisi tunasema Maveterani wakae pembeni wasubiri mechi za mazoezi,”anasema barafu.
Msanii huyo ambaye pia ni muongozaji wa filamu amedai kuwa mitaani kuna vipaji vingi lakini vinanyimwa nafasia na wasanii wakongwe ambao hawataki kabisa kutoa nafasi kwa wasanii hao ili kuleta ushindani wa kweli katika tasnia ya filamu Swahiliwood, Barafu yupo mbioni kuachia filamu yake inayokwenda kwa jina la Dala dala kutoka kampuni ya Usambazaji ya Leo Media.


TOA MAONI YAKO HAPA:

Sunday, October 6, 2013

MATOKEO YA ENGLISH PREMIER LEAGUE :


epl 1
 (story/picha millardayo)
Ligi kuu ya soka nchini England  imeendelea hii leo ambako michezo nane imepigwa .
Katika mchezo wa kwanza Manchester City waliwafunga Everton kwa mabao matatu kwa moja.
Everton walianza kufunga kupitia kwa Romelu Lukaku lakini Mabao toka kwa Alvaro Negredo , Sergio Kun Aguerro pamoja na bao la kujifunga la kipa Tim Howard yaliwapa Man City pointi Zote tatu .

ALBAM YA RAY C YAKAMILIKA RASMIN:

Nguli wa muziki wa Bongo Fleva Rehema Chalamila‘Ray C’amekamilisha albam ya nyimbo zake aliyokuwa akirekodi studio kwa miezi kadhaa.
 Kupitia mtandao wa instragram Ray C alisema kuwa….Album imekwishaaaaaaaaaaaaaaaaaa!Thank You Lord!
 Hivi karibuni msanii huyo alipost video na kuwaonjesha mashabiki wake ladha kidogo kati ya nyimbo zitakazopatikana kwenye albam hiyo ambayo haijajulikana itaitwa jina gani.
TOA MAONI YAKO HAPA:

Friday, October 4, 2013

HAPPY BIRTH DAY MTANGAZAJI WA CLOUD TV ZAMARADI MKETEMA:

Na mimi ningependa kuwa miongoni mwa wale ambao watamtakia Happy birthday Zamaradi Mketema:
Zamaradi Mketema ni Producer & Presenter wa show ya Take one (movie program) ya  Clouds Tv /clouds FM Radio..
HAPPY BIRTHDAY
TOA MAONI YAKO HAPA:

20 PERCENT NA PRODUCER MAN WATER WAYAMALIZA KIHIVI:


Hakika Nyumbani ni Nyumbani tu ...Mwanamuziki 20 Percent ambayo miaka kama miwili iliyopita alikuwa ni tishio katika muziki wa Bongo Flava Hatimae ameamua kujirudi na kuondoa Beef walilo kuwa nalo na Producer wake ambaye ndio alikuwa anamtoa Man Water ...Wawili Hao wamekuwa kwa muda mrefu hawapatani kila mtu akisema mwenzake ndio mbaya ...ila leo wamekutana katika Ofisi za Magic FM na Kumaliza Tofauti zao na Kuhaidi kufanya kazi pamoja tena...20 Percent toka aachane na Producer huyo ameshindwa kabisa kufurukuta katika Game Hilo na kuonekana ameishiwa kabisa....Tunamuombea Arudi tena kama dhamani tupate Burudani Safi toka kwake;

TOA MAONI YAKO HAPA:

Thursday, October 3, 2013

TATOO YA UWOYA YALETA MTAFARUK:

 credit/BongoMovies
Mwanadada Irene Uwoya ammepa maneno ya busara fan wake kupitia kwenye ukurasa wake wa mtandao mmoja wa kijamii hivi karibuni.
Tukio hilo lilikuja baada ya fan huyo kwa jina moja la Hellen kumuandikia Irene uwoya kuwa maneno ya kumshauri kuhusu tattoo yake ya mkononi,
kwanza kabisa mwanadada huyo alimwambia Irene kuwa anampenda sana na pili Irene kama mkristo hatakiwi kuwa na hizo tattoo kwani Mungu hapendi, ndipo Irene Uwoya alimpomjibu kuwa Mungu anaangalia moyo na sio mambo mengine:
Hellen: dada nakupenda sana....ila wew n mkristo jmn izo tattoo mungu apend cyo siri yan#irene
Irene Uwoya: Mungu anangalia moyo si tattoo”
Kama hii haitoshi fans wengine nao wakaanza kuandika..(Tukinukuu)
Kulwa: Moyo kwa maana ya matendo,tabia muonekano ama sivyo?
Piere: Hata mm mkristo na Tatoo ninazo anaesema mungu apendi kuna mstari gani kwenye vitabu vyake vitakatifu ilipoandikwa hapendi tatoo
Je ni sahihi kuchora tattoo kama alivyodai Irene au ni knyume na maagizo ya vitabu vya dini? Tupe maoni yako
TOA MAONI YAKO HAPA:

Wednesday, October 2, 2013

WEMA SEPETU KULISHTAKI GAZETI HILI?ANGALIA ALICHOANDIKA:

MWIGIZAJI wa filamu za Kibongo,Wema Sepetu ameonyeshwa kuumizwa na habari iliyoandikwa na gazeti la udaku la Filamu baada ya kuandika kuwa ameenda nchini China kuuza madawa ya Kulevya‘ unga’na kuandika waraka(ujumbe) mrefu mtandaoni kuwa amechoshwa kusakamwa kila wakati kwa kuandikwa habari za uongo juu yake.

Wema alipost ukurasa wa mbele wa gazeti hilo na kuandika …Hahahahha.. haya niombeeni watanzania.... aisee... magazeti ni noumerrr... mambo ya kunyongwa tena na wakati sufuria zina shake zenyewe... dah... this made my day...…

Tuesday, October 1, 2013

LULU AFUNGUKA YA MOYONI KWENYE SIMINA YA FURSA:


TOA MAONI YAKO HAPA:

IRENE UWOYA AMEACHANA KABISA NA KU ACT FILAM SOMA HAPA ZAIDI:



CREATIT DSTV
Mwigizaji Irene Uwoya ambae alipata tuzo ya Steps kama mwigizaji bora kike 2012/2013 amethibitisha kuacha kuigiza movie kwa sasa ili kufanya kazi ambayo ameianza hivi karibuni.

Namkariri akisema: “Nimeamua kuacha mambo ya movie na kuwaachia wengine, haya maamuzi nimeyafanya kama miezi sita iliyopita… Mara ya mwisho kuigiza ni zaidi ya miezi sita iliyopita pia.”

Irene ambae ni mama wa mtoto mmoja kwa sasa anafanya show ya TV ya kusaidia Watanzania wanaoishi kwenye nyumba ambazo ni mbovu au hazina mahitaji muhimu yanayotakiwa kwenye nyumba.

Ni show ambayo haitahusika ku....

Saturday, September 28, 2013

Hadji Adam, apata stashahada ya Sanaa ya maigizo leo toka chuo cha Bagamoyo,


Hongera Hadji Adam, apata stashahada ya Sanaa ya maigizo leo toka chuo cha Bagamoyo, ni mfano wa kuigwa
 (habri/picha na bongomovies)
Mwigizaji Hadji Adam leo amepata Stashahada yake ya maigizo ya drama na filamu toka chuo cha sanaa Bagamoyo mkoa wa pwani.
Katika mahafali hayo yaliyofanyika kwenye ukumbi wa chuo hicho Hadji pamoja na wahitimu wengine wamepata zawadi na vyeti mbalimbali toka kwa uongozi wa chuo hicho.
Akizungumza na simu tokeo Bagamoyo alipo sasa Hadji amesema kuwa anajisikia furaha sana kuhitimu mafunzo yake yake hayo na anasema kuwa hapo ni mwanzo tuu na anajiandaa tena ili aendelee na elimu zaidi.
“kwakweli nina furaha sana siku ya leo, namshukuru Mungu nimemaliza salama na natumai nikipumzika nitaendelea na masomo zaidi hapo mwakani” alisema Haji.
Bongomovies.com tunapenda kumpa pongezi za dhati haji kwa hatua hii na tunamtakia kila la kheri katika masomo yake yanayokuja.
TOA MAONI YAKO HAPA:

Friday, September 27, 2013

SALAM ALIZOZIPATA WASTARA KUTOKA KWA MASTAR MBALI MBALI HIZI HAPA:

 Leo ni Birthday ya Mwanadada Wastara Sajuki ambaye kwa nyingine kama si mara ya kwanza tangu afiliwe na mumewe, utamuona kwenye Filamu Yangu mpya ya DR MAX itakayotoka hivi Karibuni: na hapo kwenye picha ni scene moja mimi na yeye:

Wastara mwenyewe amejipongeza kwa kusema...
Happy b/day 2 me""Alhamdulilah namshukuru sana m/mungu kwa kueza kunifikisha katika siku hii mpaka sasa ni mzimah""Namtanguliza yeye kwa kila jambo anisimamie katika maisha yangu""Ameen""""

Batuli:
★★You are the best person of this world, I'm sure this year gonna be your greatest★★★ happy birthday to u★★★ happy birthday to u★★★ Happy birthday dear wastara happy birthdat to uuuuuu★★★Love u Chimamy

Nisha:

Wednesday, September 25, 2013

(PICHA)HIZI PICHA ZA MWISHO BAADA YA KUMALIZA KUSHOOT FILAMU YA DR MAX::

Habari za leo watu wangu pamoja na wadau wakubwa wa blog hii, nitakua mchoyo wa fadhila km sitamshukur allah muumba kwqa kutuwezesha kumaliza salaama kabisa kushoot filam mpya ya cy&cl company inayoitwa DR MAX, Na kwa sasa zimebakia process za kitaalam tuu so kaaeni tayari, tutapeana maelezo lini inatoka rasmi na itazinduliwa wapi , kila kitu kuhusu filamu hiyo na Cloud 112 ni hapa kwenye blog yangu;
Asanteni sana kwa ushikiano wenu wa mawazo na kila kitu NAWAPENDA sana;
Angalia picha hapa za mwisho mwisho mimi na crue nzima ya CY&CL COMPANY.......

(PICHA)RAY KIGOSI KUTOKA NA FILAM HII:




(picha/storyna DJCHOKA)
Super Star wa Bongo Movie nchini Ray Kigosi aka The Greatest sasa yupo kwenye matengenezo ya movie yake mpya ambayo amewashirikisha wasanii wenzake wa bongo movie wakali katika game hili. Katika account yake ya Instagram Ray ameonekana akionyesha picha wakati wakiishuti movie hiyo pasipo kutaja jina la movie hiyo huku akiwaambia mshabiki wake wakae mkao wa kula na kuona ujio wake mwingine.

Hebu onja kidogo picha kadhaa wakati wakishuti movie hiyo hapa...

Tuesday, September 24, 2013

MBAYA WA AUNT AHENYA KORTINI

Yvonne Maximilian akiwa eneo la mahakama.
Stori: Musa Mateja GPL
Hatimaye yule mbaya wa mwigizaji wa filamu za Kibongo, Aunt Ezekiel aitwaye Yvonne Maximilian (22) amenaswa na kuhenyeshwa kortini kisa kikiwa ni kumpiga chupa mwigizaji huyo.
Yvonne aliburuzwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar baada ya kukamatwa maeneo ya nyumbani kwake Kinondoni-Manyanya..........

Sunday, September 22, 2013

DAY 3: PICHA ZA BEHIND THE SCENE ZA FILAMU YA "DR MAX" HIZI HAPA;

k
Kama kawaida fans wangu tunakutana tena tukiwa wazima wa afya Alhamdulilah, Imani yangu na nyinyi ni wazima pia kwa sababu tuu bado tunavuta pumnzi mpaka dakika hii, Ule muendelezo wa Filamu yangu ya DR MAX bado unaendelea nahizi ni picha nyengne kabisa, kuwa wewe wa kwanza kuziona kabla ya mtu mwengne yoyote ndio kwanza naziweka hapa; Na hii ni DAY 3, tulianza na DAY 1 ,tukaja DAy 2 sasa hii ni DAY 3 , Angalia hapa picha za DAY 3, behind the scene
Karibuni sana:

Saturday, September 21, 2013

HII NI BAADHI YA VIDEO YA TUKIO KWENYE SHAMBULIO NCHINI NAIROB NI HATARI SANA:

Imetoka MILLARDAYO.COM
Ni dhahiri kwamba ndugu zetu wamepata tabu sana kwa tukio hili, ni shambulio ambalo limefanya idadi ya waliofariki kufikia 39, hizi video mbili zinaonyesha baadhi ya matukio wakati wa uokoaji nje na ndani ya Westgate Mall ambapo Polisi wamesema ni zaidi ya watu 600 wameokolewa kutoka ndani.
TOA MAONI YAKO HAPA:

Thursday, September 19, 2013

DAY 2: PICHA ZA BEHIND THE SCENE ZA FILAMU YA CLOUD 112 INAITWA "DR MAX" HIZI HAPA;

Habari za leo wadau wangu wakubwa wa blog hii pamoja na filamu zangu, hopefull mko vizur SANA , na mimi nipo mzima wa afya Alhamdulilah, Bado tupo Kambini kwa ajili ya kuendelea kuishoot Filamu ya "DR MAX" kwa ajili yenu, Na Leo kama tulivyo ahidiana tutakua tukipeana picha za nyuma YA Pazia Kwa kile kinachoendelea huku, kila tutakapo kua wazima wa afya kwa mtindo wa DAY, Juzi niliweka picha na ilikua ni  DAY 1, Leo kwa taratiibu kabisa nime wawekea picha za DAY 2, Jinsi tunavyoshoot huku:
Karibu sana kuziangalia picha za DR MAX behind the scene DAY 2: Hizi hapa....

Wednesday, September 18, 2013

LULU AMEFANYA FILAMU MOJA NA MAMA KANUMBA, CHECK HILI KAVA NA ALICHOANDIKA:

Mwigizaji wa sinema za Kibongo,Elizabeth Michael(Lulu) amecheza filamu na mama wa aliyekuwa msanii wa Bongo Movies,marehemu Steven Kanumba,Frolah Mtegoa iitwayo Mapenzi ya Mungu ambayo inatarajiwa kutoka hivi karibuni.

 Lulu amepost kava la filamu hiyo kwenye mtandao wa instragram na kuandika kuwa …MAPENZI YA MUNGU....ELIZABETH MICHAEL + FLORA MTEGOHA(MAMA KANUMBA)....STAY TUNED …..
Huku baadhi ya watu wakimpongeza na kumwambia hope 448 hongera mungu azid kukuangazia .amani yake iwe juu yako,

 Hii ni mara ya kwanza Lulu kufanya filamu na Mama Kanumba tangu alipopata matatizo ya kesi ya mauaji ya msanii Kanumba na pengine kuibua maswali kwa mashabiki ni nini kimeongelewa ndani ya filamu hiyo kati ya mtu na ‘........’.
 Filamu hiyo pia imemshirikisha msanii wa Bongo Fleva,Linna Sanga.
TOA MAONI YAKO HAPA:

JOANITA ARUDI KWA KISHINDO NA FILAMU YA HARAKA YA NDOA!

(Habari / Picha: Na Ripoti Filamucentral / FC)
MWIGIZAJI wa kike Bongo Fatuma Makame ‘Joanita’ anakuja na filamu inayojulikana kwa jina la Haraka ya Ndoa, Joanita ni moja kati ya mazao ya mtayarishaji na muongozaji wa kitambo Mussa Banzi msanii huyo ambaye ni mahiri katika uigizaji anaamini kuwa moja ya sababu inayokwamisha wasanii ni mfumo wa usambazaji kwa sasa anakuja na kampuni nyingine ya usambazaji............