Pages

MY NEW FILM TRAILER INAITWA ''DR MAX''

Wednesday, April 25, 2012

Tmk, Shilole, Ferooz, Belly Black na wengine kuivamia Iringa na Songea

MENEJA wa kundi la Tmk Wanaume Family Saidi Fella, ameungana na  wasanii zaidi ya kumi na mbili katika sherehe ‘Party’  maalum siku ya burudani mkoa wa Iringa.
Saidi Fella  alisema, party hiyo itafanyika may 6  katika kiwanja cha Samora, baada ya kuombwa kufanya burudani na mashabiki baada ya kukaa muda mrefu bilayakufanya kufanya tamasha kwenye mkoa huo.
(Ferooz)
Alisema miongoni mwa wasanii ambao watakuwepo siku hiyo ni Feroozi Mrisho’Ferooz’, Zuwena Mohamedi ‘Shilole’, Berry Black, Nurudini ‘Baba Kitorondo’, Saidi Juma, ‘Chege’, Amani Temba ‘Muheshimiwa Temba, Aslay Sadiq ‘Dogo’ Aslay, Ize Man, Dogo Muu na wengine.
(Dogo Aslay)
Pia alisema hata hivyo ijumaa ya may 4 wanatarajia kundi hilo lote kufanya tamasha mkoani Songea katika ukumbi wa jambo Lee wakati mchana watakuwa kwenye viwanja vya Majimaji.
Shilole
Bibi Cheka atakuwemo

No comments:

Post a Comment