Pages

MY NEW FILM TRAILER INAITWA ''DR MAX''

Thursday, April 19, 2012

Hammer Q aziba pengo la MudiChriss Offside Trick

Wanazmuziki ambao wanaunda kundi la Offside Trick, mmoja wapo ameamua kujitoa na inasadikiwa kwamba ameachana kabisa na masula ya muziki. Kiongozi wa kundi hilo lenye makazi yake Zanzibar ila kwa sasa wamehamia Kigamboni jijini Dar es salaam, ambao maarufu kwa  kwa kupiga muziki wa mduala, ambalo linatamba na nyimbo kama Dege, Bata, na Hammada, amesema kwamba mwenzake kwa sasa yupo Zanzibar anaendelea na kazi zingine. Anasema msanii mwenzake ambaye amejitoa ni Mudatiri Masudi ‘Mudi Chriss’. lakini amesema baada ya kuondoka kwa Mudi Chriss kwa sasa nafasi yake imechukuliwa na mwanamuziki kutoka pande za hukohuko, Hammer Q,ambaye naye alishavuma na nyimbo za taarabu kama vilePembe la Ng'ombe. (Picha ya juu ni Lil Ghetto na Hammer Q)

Mudi Chriss aliyejitoa Offside Trick

Kundi la Offside Trick, mwanzo kabla ya kujitoammoja wapo.

No comments:

Post a Comment