Pages

MY NEW FILM TRAILER INAITWA ''DR MAX''

Wednesday, October 2, 2013

WEMA SEPETU KULISHTAKI GAZETI HILI?ANGALIA ALICHOANDIKA:

MWIGIZAJI wa filamu za Kibongo,Wema Sepetu ameonyeshwa kuumizwa na habari iliyoandikwa na gazeti la udaku la Filamu baada ya kuandika kuwa ameenda nchini China kuuza madawa ya Kulevya‘ unga’na kuandika waraka(ujumbe) mrefu mtandaoni kuwa amechoshwa kusakamwa kila wakati kwa kuandikwa habari za uongo juu yake.

Wema alipost ukurasa wa mbele wa gazeti hilo na kuandika …Hahahahha.. haya niombeeni watanzania.... aisee... magazeti ni noumerrr... mambo ya kunyongwa tena na wakati sufuria zina shake zenyewe... dah... this made my day...…


 Staa huyo katika ujumbe huo aliandika kuwa hawezi sema kwamba yuko happy na kwamba hakuwahi kufikiria kuwa hata siku moja magazeti yanaweza kuandika uongo mkubwa wa namna hiyo na huwa anakaa kimya na kuaona kuwa wanaweza kumuonea muda wote na roho inamuuma sana na amechoka kuchafuliwa jina bila sababu za msingi.

Swali linakuja Je?Wema atachukua hatua gani dhidi ya gazeti hili maana amekuwa akiandikwa sana lakini hajawahi kuzungumza kama ameumia kiasi hiki
Wema yupo nchini China kwa siku kadhaa akifanya shughuli zake ambapo pia alingusha bonge la pati katika sherehe ya kuzaliwa kwake akiwa na marafiki zake akiwemo msanii mwenzake Aunt Ezekiel.
TOA MAONI YAKO HAPA:

No comments:

Post a Comment