Pages

MY NEW FILM TRAILER INAITWA ''DR MAX''

Tuesday, May 15, 2012

King Majuto apata shavu Azam

Lile nguli la filamu za kuchekesha  Tanzania,  Athuman Majuto ‘ King Majuto’, hivi karibuni aliingia mkataba na wauzaji wa bidhaa za Azam, na kumchukuwa akiwa kama Balozi mpya wa bidhaa hizo huku akishirikiana na  Hussein Kiety 'Sharo milionea' katika kazi zake. Majuto alisema mkataba na kampuni ya  Al – riyami ameuvunja kwa kuwalipa shilingi milioni 20.  Alisema kampuni ya Al - riyami kwa sasa imekuwa  inarusha kipindi cha Vituko Show zile ambazo aliigiza zamani wakati yupo nao.
“Sasa hivi kazi zote nitakuwa nikizifanya kwaajili ya bidhaa za Azam, pia nipo kwenye mikakati mingi juu ya kazi zangu mpya” alisema.
Hata hivyo King Majuto kwa sasa kazi zake atakuwa akifanya Dar es salaam na akimaliza anarudi Tanga ambapo kazi zake zingine zinaendelea, wakati huo huo katika kampuni hiyo anaenda kukutana na mzee Small ambaye amekuwa akitangaza bidhaa za kampuni ya Azam kama vile tui la nazi katika bidhaa ya Azam.

1 comment:

  1. blog yako iko poa sana Cloud
    jacque belgique

    ReplyDelete