Pages

MY NEW FILM TRAILER INAITWA ''DR MAX''

Wednesday, September 12, 2012

Kalala Junior kuzunguka mikoa

BAADA ya bendi mama ya wanamuziki wengi ya Twanga Pepeta, kumrudisha kundini mwanamuziki aliyekuwa akifanya vizuri katika bendi ya mapacha watatu, Kalala Junior, imeamua kufanya harakati zake za mikoa ya Iringa na Mbeya.

Siku ya kwanza Twanga Pepeta inataraji kufanya onyesho mkoani Iringa tarehe 14-09-2012 siku ya Ijumaa katika ukumbi wa Highland.
Kesho yake siku ya Jumamosi tarehe 15-09-2012  watakuwa Jijini Mbeya ndani ya City Pub na siku ya Jumapili tarehe 16-09-2012 watamalizia kufanya ziara ya maonyesho katika ukumbi huo huo wa City Pub  kwa kufanya Bonanza maalum kwa ajili ya wakazi wa Jiji la Mbeya na maeneo ya jirani.
Matayarisho yote muhimu ya ziara hii ya maonyesho yamekamilika na Bendi inataraji kuondoka mara baada ya kumalizika kwa onyesho la kila siku ya Alhamisi tarehe 13-09-2012 linalofanyika Club Maisha Oysterbay.
Bendi inataraji kurudi mara tu baada ya onyesho la mwisho litakalofanyika siku Jumapili tarehe 16-09-2012 Jijini Mbeya.
Twanga Pepeta itakapokuwa katika ziara, Itamtambulisha Mwimbaji wao mpya Kalala Jr aliyerejea hivi karibuni kutoka katika Bendi  ya Mapacha Watatu.
Sambamba na utambulisho huo pia itatambulisha nyimbo zao mpya za “Ngumu Kumeza” ilyotungwa na  Mirinda Nyeusi, “Nyumbani ni Nyumbani” iliyotungwa na Kalala Jr, “Walimwengu” iliyotungwa na Jumanne Said  na ” Mapambano ya Kipato” iliyotungwa na Mwinjuma Muumini.
Mara baada ya kurejea Twanga Pepeta itaendelea kufanya maonyesho yake kama kawaida Jijini Dar es salaam katika kumbi za Club Billicanas siku ya Jumatano, New Club Maisha siku ya Alhamisi, Free Time Resort Ukonga Banana, Mango Garden siku ya jumamosi na Jumapili mchana Leaders Club na usiku Mzalendo Pub.
MUDDY K
EVENTS MANAGER

No comments:

Post a Comment