Pages

MY NEW FILM TRAILER INAITWA ''DR MAX''

Monday, August 6, 2012

Machapa watatu wajipanga kivyao


BENDI ya dansi nchini ya Mapacha Watatu, kuondokewa na mwanamuziki wao Kalala Junior, wameachai wimbo mpya wa Ona Naonewa huku wakijiandaa na ujio wa albamu yao ya pili.
Mmoja wa wanamuziki wa bendi hiyo Jose Mara, alisema kwamba wimbo huo wamemshirikisha Ali Kiba pamoja na Kharidi Chokoraa utakuwa kwenye albamu hiyo ambayo itakuwa na nyimbo 7.
Aidha alisema kwamba jina la la albamu hiyo, amemwachia Chokoraa kwakuwa albamu ya kwanza alishatoa yeye jina, pia alishatuka wimbo kama usio wa baba na huu wa Ona naonewa.
“Ujue kupeana nafasini jambo la muhimu, hivyo jina  la albamu hii itatoka katika wimbo ambao atautunga yeye” alisema.
Pia alisisitiza kusema bendi hiyo, haitachukua mwanamuziki mkongwe kuogopa lawama, ila itachukuwa wanamziku chipukizi.

No comments:

Post a Comment