Pages

MY NEW FILM TRAILER INAITWA ''DR MAX''

Friday, March 9, 2012

FASHA JOSHUA ARUDI UPYA


FASHA JOSHUA

Mwanamuziki aliyekuwa Dubai Fasha Joshua amerudi upya katika bendi yake ya Twanga Pepeta, ilikuziba nafasi  iliyoachwa na mwanadada ambaye alikuwa mnenguaji wa kundi hilo Lilian Internet, ambaye kwa sasa ameamua kuhamisha makazi yake hadi Mashujaa kwa kina Chaz Baba. 

Kiongozi wa kundi la Twanga amesema amepokea taarifa za kuhama kwa mnenguaji wake huyo, lakini kwao haikuzuru kwakuwa tayari wanaye mnenguaji mwingine ambaye alikuwa likizo Uarabuni. 

Wanenguji wa Twanga Kazini

Twanga Pepeta

Uongozi wa Twanga wamesema mnenguaji wao ameanza kazi rasmi jumatano hii, hivyo taratibu kazi zake zitaanza kuwa wazi mbele ya mashabiki wake. 

Haya kwa wale ambao ni wapenzi wa Twanga kazi hailali mambo  ni bandika bandua na kata funua, kazi kwenu.....

HALUUUUAAAAAAA!

No comments:

Post a Comment